Elimu ya Afya ya Jamii

Afya Ya Jamii

Afya Ya Jamii


Jifunze njia za kujikinga na maambukizi ya Ebola.


Jinsi ya kujikinga na ugonjwa wa Ebola :

Epuka kusalimiana kwa kushikana mikono au kukumbatiana

Epuka kugusa damu, matapishi, mkojo, kinyesi, kamasi, mate, machozi na maji maji mengine yanayotoka mwilini mwa mtu mwenye dalili za ugonjwa huu

Epuka kugusa au kuosha maiti ya mtu aliyekufaakiwa na dalili za ebola badala yake toa taarifa kwa uongozi wa serikali ili wasimamie taatibu za mazishi

Epuka kutumia nguo, shuka, blanketi, kitanda nagodoro za mtu aliyeambukizwa ugonjwa, toa taarifa kwenye ofisi za serikali ya eneo husika

Kwa kuwa ugonjwa huu pia huambukizwa kwa njia ya kujamiiana, epuka kuwa na mpenzi zaidi ya mmoja

Nawa mikono kwa maji yanayotiririka na sabuni mara unapomtembelea mgonjwa hospitalini au kumhudumia nyumbani

Epuka kugusa wanyama kama vile Popo, Nyani, Sokwe, Tumbili na Swala au mizoga ya Wanyama

Zingatia ushauri na maelekezo yanayotolewa na wataalamu wa afya na viongozi wa serikali.

Wahi kituo cha kutolea huduma za afya uonapo dalili za ugonjwa wa Ebola

Toa taaifa mapema kwa watoa huduma za afya uonapo mtu mwenye dalili za ugonjwa wa Ebola au kifo

Zingatia usafi binafsi pamoja na usafi wa mazingira yako.


read more